IQNA

Kadhia ya Palestina

Polisi  Saudia wamkamata Muiraqi aliyemuomboa dua Shahidi Haniya huko Makka

20:39 - August 06, 2024
Habari ID: 3479234
IQNA - Vikosi vya usalama vya Saudi Arabia vimeripotiwa kumkamata profesa wa chuo kikuu kimoja cha Iraq katika mji mtakatifu wa Makka kwa kosa la kutoa kumuomboea dua kiongozi wa Palestina Ismail Haniya aliyeuawa shahidi wiki iliyopita katika hujuma ya kigaidi ya Israel

Profesa, Salman Dawood al-Sabawi alimuomboea dua shahidi Haniya wakati alipokuwa akifanya ibada ya Hija ndogo, Umrah, kulingana na ripoti ya Press TV.

Taarifa za wanaharakati katika mitandao ya kijamii hasa X zinaonyesha  picha za Sabawi akiwa ameshikilia bendera ndani ya eneo la  Masjid al-Haram, eneo takatifu zaidi  katika Uislamu. Bango lilisomeka, "Naizawadia Umra yangu hii kwa shahidi Ismail Haniya" kwa Kiarabu.

3489388

Kufuatia habari za kuzuiliwa kwa Sabawi, watumiaji wengi wa mitandao ya kijamii waliingia kwenye X, Facebook, na majukwaa mengine, wakitaka aachiliwe mara moja na bila masharti. Sabawi ni mkazi wa mji wa Mosul, kusini mwa Iraq.

Ismail Haniya, ambaye alikuwa Tehran kuhudhuria sherehe za kuapishwa kwa rais mpya wa Iran, Masoud Pezeshkian, aliuawa shahidi pamoja na mlinzi wake katika shambulio la Israel mapema Julai 31.

Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Seyyed Ali Khamenei ameuonya utawala wa Israel kuhusu "jibu kali" kwa mauaji ya Haniya na kusema kuwa ni jukumu la Jamhuri ya Kiislamu ya kulipiza kisasi damu ya kiongozi wa mapambano ya Palestina.

"Utawala wa Kizayuni wa jinai na kigaidi ulimuua shahidi mgeni wetu mpendwa katika nchi yetu na kutuacha tukiwa tumefiwa, lakini pia ulijiwekea uwanja wa adhabu kali," amesema Kiongozi Muadhamu.

Habari zinazohusiana
Kishikizo: ismail haniya shahidi
captcha